Breaking News

Sep 20, 2025

MGOMBEA UBUNGE ATOA MATUMAINI MAPYA KWA WANANCHI MOROGORO KUSINI

Mgombea ubunge Jimbo la Morogoro Kusini,Zuberi Mfaume

Na Thadei Hafigwa

WANANCHI wa Jimbo la Morogoro Kusini wameanisha kero na kuziwasilisha kwa Mgombea ubunge kwa tiketi cha chama cha Mapinduzi,Zuberi Mfaume ili zipatiwe ufumbuzi ikiwemo changamoto za miundombinu ya barabara,maji, uchungaji holela wa mifugo ilinayoharibu mazao ya wakulima shambani husuan kipindi cha kilimo.

Wakazi wa Kata ya Selembala,Kisaki,Mvuha,Mngazi na Bwakila chini Morogoro vijijini wamebainisha hayo kwa nyakati tofauti kwenye mikutano kampeni inayoendelea jimboni humo ambapo wameonesha imani walionayo Mgombea ubunge wa ccm jimbo la Morogoro kusinijambo lililowalazimu wagombea wengine kutoka vyama vingine vya kisiasa walionesha nia ya kuwania nafasi ya ubunge wa jimbo hilo  kutorudisha fomu walizochukua tume huru ya taifa ya uchaguzi.

Zuberi Mfaume ni Mgombea pekee ubunge Jimbo la Morogoro kusini kwa tiketi ya CCM ambaye Oktoba 29, 2025 siku ya Kupiga kura atapigia kura ya Ndiyo au Hapana kwenye kinyang’anyiro hicho.

Wagombea nafasi ya udiwani na Mgombea Ubunge,Jimbo la Morogoro Kusini,Zuberi Mfaume wakiwa katika picha ya pamoja baadhi ya viongozi wa ccm wilaya ya Morogoro vijijini,mara baada ya kumaliza harakati za kunadi Ilani ya CCM 

Mfaume akiwa katika mikutano yake ya kampeni katika kata ya Selembala,Mvuha,Kisaki,Mngazi na Bwakila Juu, amejitwika mzigo wa changamoto zinazowakabili wananchi wa  maeneo hayo ambazo ni miundombinu ya barabara,uchungaji holela wa mifugo ambayo inaharibu mazao ya wakulima,stakabadhi ghalani pamoja na pungufu wa maji katika maeneo ya vijijini ambayo kwa mujibu wa sera ya maji,inayoelekeza wakazi wa vijijini wanapaswa kufikiwa huduma ya usambazaji wa maji kwa asilimia 85.

amewahakikishia wananchi wa maeneo hayo kuwa changamoto zinazowakabili zitashughulikiwa mara  baada ya kuchaguliwa kuhudumu nafasi ya ubunge kwa kuwa tayari ashaandaa mkakati maalum wa kuzipatia ufumbuzi changamoto zilinazowakabili  wananchi,.

“kipaumbele changu cha kwanza nitaimarisha ofisi ya mbunge kwa kuweka  dawati la msaada wa sheria ili kuwasaidia wananchi kukabiliana na changamoto za kisheria”alisema.

Mgombea huyo mbali na taaluma nyingine alizonazo pia ni mwanasheria, alinukuu ahadi iliyoanishwa kwenye Ilani ya CCM 2025-2030 iliyoelezea utatuaji wa changamoto ya miundombinu ya barabara kutoka ubenazomozi hadi Mvuha.

“ahadi namba 265 katika Kitabu cha Ilani ya chama cha Mapinduzi unasomeka Mradi wa upembuzi yakinifu katika barabara ya Ubenazomozi, Ngerengere, kuelekea kituo cha SGR,Tununguo,Selembala,Mvuha inaungana na Bigwa Kisaki kuelekea bwawa la Mwalimu Nyerere itajengwa katika kiwango cha lami”.

Harakati za kampeni zinapopamba moto viongozi wa ccm wakipongezana na Mgombea ubunge wa Jimbo la Morogoro Kusini,Zuberi Mfaume

Rajabu Changa ni wakili msomi wa Mahakama kuu Tanzania, katika maoni yake ameshauri namna ya kutatua migogoro mingi iliyopo katika maeneo ya vijijini inatokana na kukosekana kwa uwelewa katika masuala ya sheria hususan sheria ya Ardhi na.4 ya mwaka 1999 na sheria ya KIjiji na.5 ya mwaka 1999.

“pamoja kutambua sheria hiyo ya ardhi na vijiji katika kutatua changamoto za migogoro ya ardhi inapaswa wanakijiji kuunda sheria ndogondogo na kutambua Sheria ya serikali za Mitaa,Mamlaka ya Wilaya,Sura 287 toleo la mwaka 2023,kwamba kifungu  cha 170 kinaeleza Mamlaka ya serikali ya Kijiji kutunga sheria zake,village by laws”alisema.

Alibainisha ya kuwa,Kata ya Selembala imeingizwa katika barabara kuu inayotoka Ubenazomozi mpaka  Mvuha ambayo tayari imeingizwa katika upembuzi yakinifu ili ijengwe kwa kiwango cha rami,kwamba imetafsiriwa kama barabara kuu kuelekea katika bwawa kubwa la kufufua umeme,Bwawa la Nyerere.

Pia, Mgombea Ubunge Jimbo la Morogoro Kusini ameahidi kushughulikia changamoto ya miundombinu ya barabara kutoka eneo la getini hadi Kijiji cha Kiganila kilichopo kata Selembala kwa kutumia mfuko wa jimbo.

“ninataka kuwaahidi kwamba serikali ya Chama Cha Mapinduzi ilitenga fedha maalum ya mfuko wa jimbo,moja ya kazi zake ni kutatua changamoto kama hizi,nitakuja kuwashukuru,tutakaa pamoja na tutaona namna gani tutapitisha greda walau barabara yetu iweze kupitika”alisema.

Kikosi kazi cha Chama cha Mapinduzi wakiwa na Mgombea ubunge wa Jimbo la Morogoro Kusini,Zuberi Mfaume wapili kutoka kushoto aliyevaa shati la Kijani mwenye miwani

Aidha,alianisha changamoto nyingine ni changamoto ya vijiji viwili Bwilachini na Kibulumo vilipitiwa na mradi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere toka mwaka 2019 wananchi wa vijiji hivyo hawana uongozi baada ya kupatiwa eneo lingine la kuishi, la mjipya.

Mzee Zuberi Mwenegoha diwani mstaafu wa Kata ya Selembala anasema kwa sasa wananchi wanasubiri maelekezo ya uongozi wa CCM Mkoa wa Morogoro ambao wameahidi kulishughulikia suala hilo.

“kwa sasa tunasubiri uongozi wa chama cha mapinduzi Mkoa wa Morogoro ambao wameahidi kuja kututembelea na kusikiliza kero zetu ili zipatiwe ufumbuzi kwa kuwa ndicho chama chenye dola”alisema Mzee Mwenegoha.

Katika mikutano yake amekuwa alitoa elimu ya sheria umuhimu wa kuishi bila ya kubaguana kati ya wakulima na wafugaji akinukuu katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.ibara ya 13(1).

“Watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki,bila ya ubaguzi wowote,kulindwa na kupata haki awa mbele ya sheria.”

Hoja hiyo imekuja baada ya wananchi kuelezea kero walionayo ya mifugo kuingia kwenye mashamba ya wakulima na kuharibu mazao. “Mkulima hana haki ya kuugua mifugo ya wafugaji,wala mfugaji hana haki ya kuingiza mifugo yake kwenye mashamba ya wakulima na kuharibu mazao.”alisema.

Aliwaahidi wananchi kumwamini kero zinazowatatiza zitawekewa utaratibu maalum wa kuzishughulikia sanjaria na kuzingatia sheria za nchi bila ya kumuonea mtu yeyote.

Temotheo Tapo kutoka jamii ya wafugaji mkazi wa  Kijiji cha Mgogoni,Kata ya Selembala amesema baadhi ya wafugaji kuingiza mifugo kwenye mashamba ya watu na kuharibu mazao si jambo jema,hata hivyo aliomba serikali kuhakikisha wanawawekea mazingira mazuri ya kujengea malambo yakunyweshea mifugo.

“Mifugo yetu inakosa maji,serikali imetukataza kutumia maji ya mito kunyweshea mifugo yetu.mifugo yetu pia inakabiliwa na magonjwa ya mapafu,midomo na miguu kuvimba tunahitaji majosho”alisema Tapo.

Katika ziara ya Kampeni Zuberi alimbatana na viongozi mbalimbali wa chama,Katibu wa Vijana wa Wilaya ya Morogoro vijijini,Mussa Idowa,wajumbe  wa Kamati ya Siasa Wilaya ya Morogoro vijijini, Donny Mbena,Zamoyoni Zuberi, Scolastika Salum,Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Morogoro, na Hamza Yahya mjumbe wa halmashauri kuu CCM  Mkoa wa Morogoro.

 Kwa nyakati tofauti walinadi wagombea kwenye mikutano ya kampeni ili kuhakikisha wananchi wanajitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura na wanachagua wagombea wanaotokana na chama cha mapinduzi,Samia Suluhu Hassan katika nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Zuberi Mfaume nafasi ya ubunge pamoja na madiwani wanaogombea katika kata 17 zilizopo kwenye Jimbo la Morogoro kusini.

Kwa upande wake Mjumbe wa halmashauri kuu ccm Mkoa wa Morogoro,Hamza Yahya aliwahimiza wanachama na wapenzi wa chama hicho kuhakikisha wanawahamasisha wananchi wengine wenye sifa ya kupiga kura wanajitokeza na kukipigia kura chama cha mapinduzi ili falsafa ya mafiga matatu iweze kutekelezeka kwa vitendo,kwa kuzingatia mnyororo wa uwajibikaji wa pamoja.

Jimbo la Morogoro kusini lina jumla ya kata 17 ambazo ni Mtombozi,Selembala,Bungu,Mvuha,Kisemo,Kasanga,Konde,Lundi,Kibuko,Kolero,Tawa,Kibogwa,Bwakira chini,Kisaki,Mngazi, Bwakila juu na Singisa.

No comments:

Post a Comment