WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII,DKT.ASHATU KIJAJI(MB)
MAKALA MAALUM
ZIARA YA KIMKAKATI
WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII MKOA WA MOROGORO
Na
Thadei Hafigwa
ILIKUWA
ni ziara ya kimkakati aliyoifanya WAZIRI wa maliasili na Utalii,Dkt.Ashatu
Kijaji(MB) ambapo ilitoa mwelekeo na maelekezo kwa mamlaka ya wasimamizi wa
wanyamapori Tanzania(TAWA) kwa kutaja vipaumbele kwa kuzingatia maagizo ya Rais wa Jamhuri Tanzania,Dkt. Samia
Suluhu Hassan yaweze kutekelezwa kwa vitendo kwa masilahi ya nchi.
Waziri
Kijaji amebainisha hayo mijini Novemba 24 Morogoro akiwa katika ziara yake ya
kwanza toka ateuliwe kushika wadhifa huo katika kipindi cha pili cha awamu ya
sita ya Rais Samia na kuongea na menejimenti ya TAWA,sanjari na kushiriki
kwenye hafla ya kuzindua vitendea kazi kwa menejimenti na watumishi wa taasisi
ya TAWA ambavyo ni magari 4,Pilipiki 33 na ndegenyuki ikiwa ni mkakati wa
kuweka mazingira mazuri ya utendaji kazi wao.
Dkt.Kijaji
alirejea hotuba aliyoitoa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu
Hassan wakati akizindua bunge la 13 aliyoelekeza wizara ya maliasili na utalii
na tasisi zake kuhakikisha wanaendelea kuimarisha ulinzi wa maeneo ya hifadhi
na udhibiti wa wanyamapori na waharibifu dhidi ya mali na maisha ya wananchi.
Alisema
kuwa,tayari serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan imeshaelekeza na kutoa nafasi ya
kuajili watumishi na askari wa wanyamapori ili kwenda kuwahudumia wananchi na
kupunguza kero dhidi ya wanyamapori wakali na waharibifu katika maeneo yao.
”tunatakiwa
tuendelee na ujenzi wa vituo vya ulinzi,tunatakiwa kuwa na mbinu za kisasa
zaidi,na vifaa pia vya kisasa ikiwemo ndegenyuki,ambavyo
tumezindua,tumizindua magari,tumezindua
pikipiki kwa hiyo hatuna visingizio tena kushindwa kuwahumia twendeni
tukawadumie wananchi wetu”alisema.
“hivyo
tunatakiwa kwenda kufanyakazi ya huduma kwa wananchi wetu kwa kujali utu wao”
Waziri
aliitaka menejimenti ya TAWA kujipanga katika kuhakikisha ya kuwa wanakwenda
kutekeleza maelekezo hayo kwa weledi ili watanzania kuendelea kunufaika na
rasilimali zao walizojaliwa na Mwenyezi mungu.
Aliwakumbusha
kutambua kuwa msingi wa uwepo wa taasisi ya tawa ni ulinzi wa wanyamapori bila ya kuwepo kwa
jambo hilo hakutakuwemo kwa taasisi hiyo,hivyo wanapaswa kuongeza ufanisi wa doria,itelejensia na
matumizi ya teknolojia,ndegenyuki,kisukuma mawimbi,na vifaa rafiki vya ulinzi
ili kulinda rasilimali muhimu zilizopo hapa nchini.
Aidha,mkakati
mwingine alitaja ni kuzuia kwa kiwango cha juu vitendo vya ujangili ,uharibifu
wa mazingira na biashara haramu za nyara ya serikali.
Waziri wa Maliasili na Utalii,Dkt Ashatu Kijaji(katikati) akikata utepe katika hafla ya uzinduzi wa vitendea kazi kwa maafisa wa wanyamapori mjini Morogoro alipofanya ziara ya kikazi,wengine walishiriki kushika utepe kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ta wanyamapori Tanzania(TAWA),Meja Jenerali Mstaafu,Hamis Semfuko,Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,Hamad Chande,kutoka kushoto kwa Mhe.Waziri Kijaji ni Kaimu Kamishna wa Mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania (TAWA),Mlange Kabange
Pia,alihimiza
kuendelea ushirikiano na vyombo vingine vya ulinzi na usalama ili kuhakikisha
maeneo yote chini ya tawa yanabaki salama na hakina anayeyachezea.
Suala
lingine aliloliwekea kipaumbele ni kuhusisha mifumo ya taarifa,uchaguzi na
tathmini ya matukio ili maamuzi ya kiutendaji yawe haraka,sahihi na yakiufanisi
zaidi.
Alisisitiza
na kuagiza kwamba hawatavumilia upotevu wa rasilimali za taifa,kwa kuwa Tawa
wamewezeshwa kwa rasilimali zote na
utayari wa serikali ya awamu ya sita ni mkubwa katika kuhakikisha inaendelea
kuweka mazingira wezeshi ili kurahisha
kutendaji kazi kwa urahisi zaidi.
Aidha,Waziri
huyo wa maliasilia na utalii aliwataka tawa kuimarisha mapato na uendelevu wa
taasisi kwa kujenga uwezo wa kifedha utakawezesha kulinda na kuendeleza maeneo
yote walioaminiwa na kukabidhiwa na watanzania.
Alitoa
maelekezo ya kuendelea kumaisha ukusanyaji wa mapato,kuhakikisha hakuna uvujaji
na kuongeza ufanisi wa mifumo ya kifedha,ni muhimu sana mifumo ikasomana.
Aliweka
mkazo kwa menejimenti ya tawa wa matumizi ya teknolojia katika ukusanyaji wa
mapato ndani ya taasisi na kamwe kutoruhusu ukusanyaji wa fedha zikiwa
mbichi,na kutumika zikiwa mbichi ili kuleta ufanisi na kurahisa kufanya
tathimini kilichokusanya na kutumika katika mwaka uliopita.
Kadhalika
aliwataka kuboresha fursa za uwekezaji rafiki hususan zenye tija katika
mazingira yanayowazunguka katika maeneo ya utalii wa ekolojia kwa kuweka kambi
za kitalii,utalii wa picha kwa kuonesha uwezo katika utendaji kazi.
Alihimiza
menejimenti ya tawa kuongeza juhudi ya utangazaji wa vivutio vya utalii
vilivyopo katika maeneo yote ya Tawa ili kuongeza idadi ya watalii wa ndani na
nje,kwa ubunifu mbinu gani zitakazotumika katika kufanikisha jukumu hilo na
kuibua vivutio vingine ili kufikia idadi ya watalii mil.8 kama ilivyoelekezwa
katika ilani ya ccm 2025-2030.
“ni
wazi tukafahamu bila ya mapato hakuna
maendeleo uendelevu wa taasisi yetu wala ya taifa letu,moja ya taasisi
zinazotakiwa kuongeza mapato ni pamoja na taasisi yetu(tawa)”alisema
Alisema
kila mmoja alimsikia Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia kwamba kipindi hiki ni cha kutumia rasilimali
zilizopo hapa nchini,kutumia mapato ya ndani ili kuweza kutekeleza miradi
mbalimbali ya maendeleo iliyopo nchini.
Suala
lingine alilosisitiza ni utoaji wa huduma kwa wananchi ni lazima ziweze
kuzingatia utu,kwamba dhamira ya serikali ni kuwatumia watu kwa utu,heshima na
haki,hivyo migongano katika ya watu na wanyamapori ishughulikiwe kwa haraka kwa
kutumia uadilifu,weledi na vifaa na miundombinu ilivyopo katika kuwahudumia
wananchi kwenye maeneo yao.
Alikemea
tabia walionayo baadhi ya watumishi wa tawa ya kuwataka wananchi kuchangia
gharama za mafuta.
“ipo
tabia ya kuwaambia wananchi,kama unataka nije changia mafuta,jambo hilo halipo
na katibu mkuu hili naomba ulisimamie ,mwananchi hatakiwi kuchangia mafuta ili
askari wetu akifikie mwananchi,ipo tabia kwa baadhi ya maeneo.”alisema
Awali,Kaimu
Kamishna wa Mamlaka ya usimamizi wa wanyamapori Tanzania (TAWA),Mlange
Kabange,asema wapo tayari kuteleza maagizo yote yanayotolewa na serikali katika
kuhakikisha malengo ya kuwahudumia wananchi yanafikiwa kikamilifu katika
uhifadhi wa wanyamapori.
Kabange
anasema kuwa tawa inajukumu la kusimamia mapori ya nje ya Tanapa na Ngorongoro,wanasimamia mapori ya akiba 28,na
mapori tengevu 23,yote kwa pamoja yana ukubwa wa kilometa za mraba
133,276.36,eneo hilo ni kubwa zinazidi ukubwa wa baadhi ya nchi.
Alisema
kuwa tawa wanatambua kuwa wana jukumu la kuhakikisha rasilimali za
wanyamapori zinalindwa na kwamba
wafanikio wanayopata yanatokana na serikali ya awali ya sita imekuwa ikiwapatia
fedha za kuteleza bajeti zao kwa asilimia 100 kwa mwaka wa fedha 2024/2025.
Alisema
mbali ya fedha za bajeti,Rais Samia aliwapatia fedha za kuboresha miundombinu
za utalii,katika kipindi cha oviko sekta nyingi zilitetereka, lakini tawa
walipewa fedha bil 12.9 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya utalii.
Sanjari
na hayo,alisema kuwa maafisa na watumishi wa tawa waliongezewa mshahara na
watumishi 3000 wenye sifa walipandishwa vyeo jambo ambalo ni rekodi ambayo
haijawahi kutokea toka kuasisiwa kwa tawa.
Aliishukuru
serikali kupitia Rais Samia kuwa sekta ya utalii imekuwa kutokana na filamu ya
royal tour na kupelekea mwaka jana (2024) walipata kampuni ya uwekezaji kutoka
china katika sekta ya utalii,jambo ambalo siku za nyuma halijawahi kutokea.
Aidha,alishukuru
wizara ya maliasili na utalii kwa kuandaa miongozo,sera na kanuni
zinazowarahishia taasisi kutekeleza majukumu yake sekta ya utalii wa uwindaji
na utalii wa picha.
Naye,Mwenyekiti
wa Bodi ya Mamlaka ta wanyamapori Tanzania(TAWA),Meja Jenerali Mstaafu,Hamis
Semfuko alimpongeza Rais Samia kwa kupata ridhaa ya kuongeza taifa la Tanzania
kwa kipindi cha pili cha awali ya sita,ambapo inatokana na imani waliokuwa nayo
wananchi kwake na uchapakazi wake katika sekta mbalimbali.
Meja
Jenerali Mstaafu Semfuko pia alionesha shukrani zake kwa serikali kwa kuweka
mazingira wezeshi katika utekelezaji wa majukumu ya tawa katika ulinzi na
uhifadhi wa wanyamapori na mazingira yake.
Kwa upande wake Katibu wa Wizara ya Maliasili
na Utalii,Dkt.Hassan Abbas alisema ziara waliifanya ni kutembelea jeshi la
uhifadhi kujua kazi zinafanyika,mafanikio na changamoto zilizopo kwa wananchi
wanaishi karibu na maeneo ya hifadhi na namna ya kukabiliana nazo.
Dkt.
Abbas ametaja Tanzania inaongoza kuwa na simba wengi duniani wapatao
17,000,jumla ya chui 24,000 ambapo Tanzania inaongoza Afrika na duniani,huku
idadi ya ni nyati 200,025,na tembo 60,000.