Breaking News

Feb 2, 2021

WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUWAELIMISHA JAMII JUU YA COVID 19


WAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUWAELIMISHA JAMII JUU YA COVID 19

Na Lilian Lucas

MGANGA wa Hospitali ya Mkoa wa Morogoro amewaeleza waandishi wa habari kwamba wanapaswa kutumia vema kalamu zao vema ili kuepuka kanganyiko kwa wananchi hasa kuna dhana kwamba watu wenye umri mkubwa kupata maambukizi ya covid 19.

Dk.Kusirye Ukio alisema waandishi wa habari wanategemewa sana na jamii hivyo wanapotimiza wajibu wao wa kitaaluma ni vema kalamu zao zisitumike kuwatisha jamii dhidi ya covid hasa  na badala yake kuwaelimisha vema kuzingatia kanuni za afya.

Ukio alisema kuwa waandishi wanapaswa kuwasiliana na mamlaka husika hasa wanapoandika habari zinazohusiana na afya ili matumizi sahihi ya maneno yanayohusu afya ya mwanadamu ili kuepuka mkanganyiko wa uelewa kwa jamii.

Aidha,Alisema kuwa, ugonjwa wa covid 19 una historia yake lakini, taaluma ya habari isitumike katika kuwapotosha jamii na badala yake iwaelimishe Jamii kwa kuzingatia miongozo inayotolewa na Wizara ya afya.

No comments:

Post a Comment