Breaking News

Aug 15, 2025

WANAHABARI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA SHERIA

 WANAHABARI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA SHERIA

Mwezeshaji wa mafunzo,Peter Kimath akiwasilisha mada ya usalama mitandaoni kwa wanachama wa MoroPC
Na Mwandishi wetu

WAANDISHI wahabari wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia sheria ili kuepuka kuingia kwenye migogoro wakati wa kuripoti habari kuelekea katika kipindi cha uchaguzi mkuu Oktoba 2025.

Peter Kimath,Elizabeth Tanzania na Peter Laurence ni wakufunzi waliojengewa uwezo na UTPC kwa kushirikiana na IMS kwa lengo la kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari juu ya ulinzi na usalama kwa waandishi wa habari sanjari na usalama mtandaoni na masuala ya saikolojia ya maisha kwa waandishi wa habari.

Peter Kimath amesema msingi bora wa mwandishi kufanya kazi zake vizuri bila kuingia kwenye changamoto ni kufuata sheria zinazomuongoza,kufuata sheria za nchi na kuangalia sera za chombo anachofanyia kazi kwa lengo la kulisha walaji wake kile wanachotegemea

“tunapaswa kuelewa sheria na kanuni zinazohusu uchaguzi na vyombo vya habari, kama Sheria ya Huduma za Habari (2016), Sheria ya Makosa ya Mtandao (2015) na Kanuni za Tume ya Uchaguzi.”anasema Kimath.

Halfan Diyu ni miongoni mwa washiriki wa mafunzo hayo akichangia mada

Mwandishi Nguli,Halfan Diyu anasema mafunzo haya yamekuja wakati muafaka kwani yamewakumbusha vitu vingi muhimu vya kuzingatia wakati wa kuripori habari za uchaguzi na nyingine katika jamii.

“tunaishukuru UTPC na IMS  kwa kuona umuhimu wa mafunzo haya kwetu,naamini tutayatumia vizuri katika kuripoti habari,na kufuata maadili ya kiuandishi ili kuepuka kuingia kwenye msigano.

Hamida Shariff ni miongoni mwa washiriki wa mafunzo hayo anasema kutokana na teknolojia vitu vinabadilika kila siku katika tasnia ya habari,hivyo wanahabari wanapaswa kukumbushwa kila wakati katika masuala mbalimbali ikiwemo ulinzi wa taarifa binafsi na sheria zinawaongoza.

“nimejifunza vitu vizuri vitakavyonisaidia katika utendaji wangu wa kazi kila siku ikiwemo,namna ya kulinda vifaa vyangu vya kazi,kujilinda wakati wa kuripoti habari uchunguzi,UTPC nawaomba kuendelea kutoa mafunzo kama haya kwani bado wanahabari tunachangamoto nyingi zinahitaji kutatuliwa kwa njia ya kupewa elimu".

No comments:

Post a Comment