Breaking News

Aug 14, 2025

WANAHABARI MOROGORO WAPEWA MAFUNZO KUFANYAKAZI KWA WELEDI

 WANAHABARI MOROGORO WAPEWA MAFUNZO KUFANYAKAZI KWA WELEDI 

Baadhi ya washiriki na wanachama wa MoroPc wakifuatilia kwa umakini mafunzo yalioandaliwa na UTPC kwa kushirikana na IMS.

Na Mwandishi wetu

WANAHABARI wametakiwa kuhakikisha Wanafanya kazi kwa uhuru bila hofu ya kudhuriwa.Wanalindwa dhidi ya unyanyasaji wa kimwili, kisaikolojia au kisheria.

Peter Laurence,Elizabeth Tanzania na Peter Kimath ni wakufunzi waliojengewa uwezo na UTPC kwa kushirikiana na IMS kwa lengo la kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari juu ya ulinzi na usalama kwa waandishi wa habari sanjari na usalama mtandaoni na masuala ya saikolojia ya maisha kwa waandishi wa habari.

Laurence alisema waandishi wa habari wanapaswa kuongeza umakini wanapotumia mitandao ya kijamii wakati wanapotimiza wajibu wao,kwani kutawaweka salama na kuepuka kudukuliwa kazi zao.

Peter Kimath alisema kuwa waandishi wa habari wanapaswa kupewa mazingira salama ya kufanya kazi, hasa wakati wa kuripoti katika maeneo hatarishi (kama maandamano, migogoro ya kisiasa, au vita).

Mwezeshaji Peter Laurence aliwasilisha mada huku wanachama wa Moropc walifuatilia kwa karibu.

Kimath akiwasilisha mada kwa waandishi wa habari wa Morogoro kuhusu ulinzi na usalama kwa waandishi wa habari alisema waandishi wa habari wazingatie weledi wanapotimiza wajibu wapo,pia wanapokabiliwa na changamoto na kadhia katika mazingira ya kazi,ambayo yanaviashiria hatarishi wawasiliane na viongozi wa Klabu za waandishi.

Mada ya saikolojia ya maisha katika mazingira ya waandishi wa habari iliwasilishwa na Elizabeth Tanzania ambaye aliwakumbusha waandishi wa habari kutambua jinsi athari ya Trauma (Kiwewe) na namna ya kukabiliana nayo.

Aliwaeleza waandishi wanapaswa kutambua maana ya trauma wa kuielezea kuwa ni hali ya maumivu makubwa ya kihisia au kiakili yanayosababishwa na tukio la kushtua sana, kama kubakwa, ajali mbaya, au kushuhudia vifo. Hali hii huweza kuathiri maisha ya mtu kwa muda mrefu.

Elizabeth Tanzania,Mwezeshaji akiwa makini katika kuwasilisha mada kwa waandishi na wanachamawa Morogoro.

“dalili ya trauma ni kumbukumbu mbaya zinazojirudia (flashbacks), kujitenga na watu, hofu au mshangao kupita kiasi,Kutojiamini, na kukosa usingizi”

No comments:

Post a Comment