Breaking News

Feb 2, 2021

HYDROXYCHLOROQUINE BADO HAIJATHIBITISHWA KUWA INAPONYA AU KUTIBU COVID-19

 
HYDROXYCHLOROQUINE BADO HAIJATHIBITISHWA KUWA INAPONYA AU KUTIBU COVID-19

Na Juma Mtanda

Dawa za Hydroxychloroquine na chloroquine hutumika kwa matibabu ya malaria na magonjwa mengine licha ya kuwepo kwa uvumi kuwa dawa hiyo zinaweza kuponya covid 19

Kwa mujibu wa shirika la afya duniani inaeleza kuwa, utafiti uliofanywa kuwa dawa hizo zina viashiria ya  kuweza dawa hizo zinazoweza kuwa tiba kwa COVID-19, lakini data iliyopo kwa sasa inaonyesha kwamba hazipunguzi vifo kutokana na COVID-19 au kusaidia watu walio na ugonjwa wa wastani.

Tanzania licha ya kuwa ni sehemu ya dunia ambayo inakabiliwa na covid 19 lakini wananchi wake wapo salama na wanaendelea kuchapa kazi,hii inatokana na serikali ya awamu ya tano kuwahamasisha wananchi kumrejea Mungu ili awanusuru watanzania dhidi ya ugonjwa huo.

Wananchi wa Mjini Morogoro na vitongoji vyake wamekuwa wakichukua tahadhali na umakini wa kipekee kwa kuzingatia miongozo inayotolewa na wataalamu wa afya ili kuhakikisha wanakuwa salama wakati wote licha ya kuwepo wa mwingiliano katika shughuli za kiuchumi.

taarifa hiyo ya WHO,inaeleza kuwa dawa ya Hydroxychloroquine na chloroquine zinaweza kutibu malaria na magonjwa ya kinga otokamtiki ya mwili. Hata hivyo, kuzitumia kutibu magonjwa mengine, bila uangalizi wa kimatibabu kunaweza kusababisha madhara mabaya zaidi na kunapaswa kuepukwa.

No comments:

Post a Comment