Breaking News

Feb 2, 2021

KATIBU WA UMOJA WA MATAIFA NA NDOTO ZAKE KUTOKOMEZA COVID 19

 

UN PHOTO/ESKINDER DEBEBE

KATIBU MKUU WA UN ANTÓNIO GUTERRES AKIPATIWA CHANJO YA COVID-19 KWENYE SHULE MJINI BRONX NEW YORK

KATIBU WA UMOJA WA MATAIFA NA NDOTO YA KUTOKOMEZA COVID 19

Ripota wetu,

MOROPC BLOG KWA MSAADA WA HABARI UN

 

KATIKA kuhakikisha ya kuwa  duniani inaendelea kuwa salama dhidi ya magonjwa ya mlipuko ikiwemo covid 19,Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema chanjo dhidi ya corona au COVID-19 ni muhimu ili kuhakikisha kila mtu kila mahali yuko salama dhidi ya janga hili hatari.

 

Guterres amesema hayo muda mfupi baada ya kuchomwa chanjo dhidi ya COVID-19 kwenye eneo la Brox jijini New York Marekani katika zoezi linaloendelea la kuwapa chanjo kwanza makundi ya watu walio hatarini zaidi kupata ugonjwa huo wakiwemo walio na umri wa zaidi ya miaka 65.

Kupitia ujumbe alioandika kwenye ukurasa wake wa twitter mara baada ya chanjo hiyo Guterres amesema

“Nimebahatika na ninashukuru kupata dozi ya kwanza ya chanjo yangu ya COVID-19 leo. Ni lazima tufanyekazi pamoja kuhakikisha kwamba chanjo inapatikana kwa kila mytu kila mahali. Kwa janga hili hakuna aliyesalama haki pale kila mtu atakapokuwa salama.”

Kwa hatua nyingine, wakazi wa Manispaa ya Morogoro wamehamasika kufuata kanuni za afya zilizotolewa na wadau mbalimbali wa afya kwa kunasa maji tiririka ili kukabiliana na magonjwa ya mlipuko ikiwemo covid 19.

No comments:

Post a Comment