Breaking News

Jan 19, 2021

TAKUKURU PWANI YAOKOA ZAIDI YA MIL.58 KATIKA OPERESHENI ZAKE


NAIBU MKUU  WA TAKUKURU MKOA WA PWANI, SADIKI  NOMBO AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI  (HAWAPO PICHANI)

TAKUKURU PWANI YAOKOA ZAIDI YA MIL.58 KATIKA OPERESHENI ZAKE

VICTOR MASANGU, PWANI   

TAASISI ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Mkoa wa Pwani imefanikiwa kuoko zaidi ya shilingi milioni 58, ambazo zimetokana na malalamiko yaliyowasilishwa yakiwemo ya wimbi la ubadhilifu wa fedha ambazo wamedhulumiwa  wakulima  wa  zao  la  korosho ikiwemo vikundi vya vijana wanawake na walemavu.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake, Naibu mkuu  wa Takukuru Mkoa wa Pwani, Sadiki  Nombo,katika utekelezaji wa majukumu yao katika kipindi cha miezi mitatu(robo mwaka) kuanzia mwezi Octoba hadi kufikia Disemba mwaka 2020 pamoja na mikakati waliyojiweke katika kukabiliana na wimbi la rushwa.

Aidha, alifafanua kuwa katika robo ya kuanzia mwezi octoba  hadi disemba mwaka 2020 Ofisi ya Takukuru iliweza kupokea mamalamiko yapatayo 196,  ambapo kati ya hayo  malalamiko 113 uchunguzi wake bado endelea kufanyika ili kuweza kuwabaini wale wote waliohusika na sheria iweze kufuata mkondo wake.

Pia, alielekeza kuwa katika utekelezaji huo, Takukuru Wilaya ya Mkuranga waliweza kuokoa kiasi cha shilingi milioni 18 ambazo zilizotoka na baadhi ya wakulima kudhulumiwa na viongozi wa bodi ya Amcos ya kimanzichana kusini.

Kadhalika, katika Wilaya ya Kibiti Takukuru iliweza kuokoa kiasi cha shilingi zaidi ya shilingi milioni 18 ambazo ziliweza kuokolewa kutoka katika vikundi mbalimbali ikiwemo kwa vijana, wanawake pamoja na walemavu ambavyo vilikopeshwa na halmashauri hiyo kushindwa kurejesha mikopo hiyo.

Alifafanua kuwa, kupitia katika Ofisi ya Wilaya ya Kisarawe waliweza kufanya uchunguzi wa kina na kuweza kuokoa zaidi ya shilingi milioni nne ambazo ziliweza kuchangwa na wananchi wa kijiji cha Marui Ngwata,kwa ajili ya kufanya ujenzi wa mradi wa Zahanati ya kijiji hicho.

Kwa upande wa Ofisi ya Chalinze, katika kipindi cha mwezi octoba hadi disemba mwaka 2020 iliweza kufanikia kurejesha kiasi cha shilingi milioni moja zikiwa ni sehemu ya shilingi milioni tano ambazo zimetokana na mikopo ambayo ilitolea kwa vikundi vya wanawake vijana pamoja  na watu wenye ulemavu.

Ofisi ya Takukuru, Wilaya ya Kibaha, waliweza kufanya uchunguzi na kuweza kuokoa zaidi ya shilingi milioni tisa kutoka kwa wanunuzi wa dawa za kituo cha afya cha Mlandizi ambapo manunuzi hayo yalikiukwa na utaratibu  haukuzingatiwa ipaswavyo kwani dawa ziliozagizwa kutoka kampuni binafsi ya Astra Pharma Limited.

Katika hatua nyingine, Naibu huyo alibainisha kwamba, Takukuru katika  kupambana  na wimbi la rushwa ya ngono ambayo imeonekana kuwa ni changamoto  kubwa katika baadhi ya maeneo hususan kwa wanafunzi wameanzisha kampeni maalumu ambayo itaweza kusaidia  kwa kiasi kupunguza  hali hiyo.

Takukuru Mkoa wa Pwani katika robo ya tatu kuanzia mwezi octoba hadi disemba mwaka 2020  imeweza kupokea  kesi zipatazo 27 ambazo zinaendelea kusikilizwa katika mahakama mbalimbali  pamoja na  kupokea malalamiko   yapatayo 196 ambapo kati ya hayo malalamiko 113 yapo katika hatua ya uchunguzi.

No comments:

Post a Comment