MBUNGE VITI MAALUM MKOA WA PWANI,MHE.HAWA MCHAFU
MBUNGE HAWA AHAMASISHA ULAJI WA MATUNDA KWA WANAFUNZI PWANI
NA VICTOR MASANGU, PWANI
MBUNGE wa viti maalumu, Mkoa wa Pwani, kupitia tiketi ya Chama Cha
Mapinduzi ,Hawa Mchafu amewahimiza wanafunzi wa shule za msingi na sekondari
kuhakikisha kwamba wanajenga tabia ya kula matunda ambayo yameoshwa na maji
safi na salama pamoja na kunawa mikono yao kwa lengo la kuweza
kuthibiti hali ya mlipuko wa magonjwa mbali mbali ambayo wanaweza kuyapata.
Mhe.Hawa alisema hayo, wakati akizungumza kuhusiana na mikakati
yake aliyojiwekea katika masuala mbalimbali ya kuboresha sekta ya
elimu ambapo alibainisha kuwa wanafunzi wanapaswa kuwa ana afya njema wakati
wote hivyo wanatakiwa kuzingatia taratibu zote ambazo zinatolewa na wataalamu
wa afya ili kuepeukana na mlipuko wa magonjwa hayo.
Mhe.Mbunge Viti Maalumu,Mkoa wa Pwani,Hawa Mchafu (katikati) akiwa katika moja ya shughuli zake za kuhamasisha maendeleo kwa wananchi mkoani humo.
“Kwa sasa hivi katika baadhi ya maeneo kuna shule ambazo zina
miti ya matunda mbali mbali hivyo wakati mwingine yanawez kuanguka chini na
baadhi ya wanafunzi waneweza kuyaokota na kula pasipo kuyaosha lakini mimi
nichukue fursa hii kuwaasa wawe na utaratibu wa kuosha mikono yao pamoja na
kuosha matunda hayo hii itasaidia zaidi katika kujikinga na magonjwa,”alisema Hawa.
Pia,Mhe. Hawa, aliongeza kuwa katika kuunga mkono juhudi za
serikali katika kupambana na mlipuko wa magonjwa mbali mbali atashirikiana bega
kwa began a walimu pamoja wataalamu wa afya ili waweze kutoa mafunzo juu ya
umuhimu wa kunawa mikono wakati wa kula pamoja na kuachana na tabia ya kula
matunda au vyakula ambayo hayijaoshwa.
Kadhalia aliongeza kuwa lengo la serikali ya awamu ya tano ni
kuhakikisha kwamba wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wanasoma katika
mazingira ambayo ni rafiki na wakiwa katika afya nzuri hivyo ni vema kukawa na
mipango madhubuti katika suala zima ya usafi wa mazingira katika maeneo mabali
mbali hususan katika ulaji wa vyakula.
Katika hatua nyingine aliwakumbusha wanafunzi hao pia kuhakikisha
kwamba wanakunywa maji ambayo yamechemshwa ili kuondokana na kupata magonjwa
mbalimbali ikiwemo kuumwa na matumbo na ambayo mengine yanakuwa na uchafu
ambao unaweza kupelekea kusababisha madhara makubwa ya kiafya.
Pia, Mbunge Hawa, aliahidi kuendelea kushirikiana na
wananchi pamoja na wataalamu wa afya katika kuweka mipango madhubuti ya kutoa
elimu ya mara kwa mara hasa katika maeneo ya vijijini ili kuweza kutoa elimu
ambayoitaweza kuwa ni moja ya msaada na mkombozi mkubwa wa kuwasaidia wananchi
kujikinga na magonjwa ya mlipuko.


No comments:
Post a Comment