Breaking News

Dec 26, 2020

PADRI KANISA KATOLIKI AKEMEA UKATILI WA KIJINSIA


Padre Lazarus Vitalius Msimbe mwenye vazi jeusi,Msimamizi wa Kitume Jimbo Katoliki la Morogoro.


PADRI KANISA KATOLIKI AKEMEA UKATILI WA KIJINSIA

Thadei Hafigwa

WATANZANIA wametakiwa kuacha vitendo vya ukatili wa kijinsia,ulawiti,ubakaji dhidi ya mtoto wa kike kwani ni chukizo kwa Mungu hasa katika kipindi cha kusherekea sikukuu ya Krismas.

Msimamizi wa kitume Jimbo Katoliki la Morogoro,Padre Lazarus Masimbe alitoa rai hiyo wakati akitoa salamu za sikukuu ya Krismas kwa mwaka 2020 katika misa takatifu iliyofanyika katika Kanisa kuu la Mtakatifu Patrick,ibada iliyohudhuriwa na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Loata Ole Sanare.

Padre Msimbe alisema kuwa vitendo vya kikatili na vya kinyama vilianza kushamiri katika vita ya kwanza na pili duniani ambapo katika kipindi hicho watu wamekuwa wakifanya matukio ya kikatili na kumchukiza Mwenyezi Mungu.

“Kitendo cha kuwafanyia ukatili watoto,utoaji wa mimba ni chukizo kwa Mungu ni sawa na dhambi ya uaji,hivyo jamii tunapaswa kubadilika kifikra ili kuzaliwa na Kristu Yesu upya” Aliasa.

Aidha,aliwataka kila mtanzania kwa nafasi yake kuwalinda watoto kwa kile alichokieleza kwamba matukio ya ukatili wa jinsia dhidi ya watoto unafanywa na ndugu wa karibu na wanafamilia.

Alisema kuwa sherehe ya Krismas haitakuwa na maana yoyote iwapo vitendo vya kikatili kwa watoto vikiwa vinaendelea kushamiri katika jamii za watanzania pia alishukuru viongozi wa serikali kwa jitihada mbalimbali wanazozifanya dhidi ya matukio ya aina hiyo.

Hivi Karibuni, Papa Francisko, alimteua Padre Lazarus Msimbe, kutoka Shirika la Kimisionari la Mungu Mwokozi (Salvatorian), Kuwa Msimamizi wa Kitume Jimbo Katoliki la Morogoro.


No comments:

Post a Comment