Breaking News

Feb 2, 2021

HALI YA JOTO , UNYEVUNYEVU NI KIBOKO CHA COVID 19?

 

MWONEKANO WA VIRUSI VYA COVID 19 KATIKA CHUMBA CHA MAABARA.

HALI YA JOTO , UNYEVUNYEVU NI KIBOKO CHA COVID 19?

Na Natharine Ugulumo

WATAFITI duniani wanaendelea na ’ kupanoa bongo’ dhidi ya kutafuta ufumbuzi wa homa ya mapafu covid 19,ugonjwa ambao unaendelea kuisumbua dunia.

Baadhi ya watu walikuwa na hisia ya kuwa kuenea kwa Covid 19 inategemeana na hali ya hewa joto au baridi,lakini watafiti na wataalamu nawaeleza kuwa  Unaweza kupata COVID-19 licha ya hali ya hewa ya jua au joto jingi iliyopo katika eneo husika.

Nchi zilizo na hali ya hewa ya joto zimeripoti visa vya COVID-19. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa njia bora ya kujilinda dhidi ya COVID-19 ni kukaa mbali na wengine na kusafisha mikono yako mara kwa mara na ipasavyo.

Nchini Tanzania kupitia wizara ya afya, maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto kipindi cha covid 19 imeweza kufanikiwa kutoa elimu kwa wananchi kuendelea kuchukua tahadhali ya kutosha kwa kuzingatia misingi ya afya kwa kunawa maji tiririka mara kwa mara si kwa kupambana na covid 19 pekee bali pia kujikinga na magonjwa ya mripuko ikiwemo homa ya matumbo,kuhara na kutapika.

Pia, wananchi kwa imani zao walikesha kuomba Mungu kwa sala na dua kwenye misikiti na makanisa,hali hiyo imesaidia Tanzania kutokuwa na athari kubwa ya covid 19

No comments:

Post a Comment