Breaking News

Mar 18, 2025

MIAKA 4 YA DHAHABU YA RAIS SAMIA KUADHIMISHWA MOROGORO

 

Mkuu wa idara ya uhusiano wa kimataifa,vyuo vya kati na vyuo vikuu UVCCM,Emanuel Martine.

MIAKA 4 YA DHAHABU YA RAIS SAMIA KUADHIMISHWA MOROGORO

Na Thadei Hafigwa

KONGAMANO kubwa la vijana la kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kutimiza miaka 4 toka aingie madarakani linatarajia kufanyika mjini Morogoro Machi 19 mwaka huu na kuhudhuria wa mawaziri mbalimbali wa kisekta.

Mkuu wa idara ya uhusiano wa kimataifa,vyuo vya kati na vyuo vikuu UVCCM,Emanuel Martine amebainisha hayo mjini Morogoro wakati akiongea na waandishi wa habari kuelezea umuhimu wa kongamano hilo ambalo Waziri wa Mipango Dkt.Kitila Mkumbo anatarajiwa kuongoza timu ya mawaziri mbalimbali wa kisekta kuelezea jinsi mafanikio yaliopatikana katika kipindi cha miaka 4 ya uongozi wa Rais Samia kwa vijana.

Martine amesema kuwa Rais Samia amefanya mambo mengi hivyo anapaswa kupewa maua yake hasa kwa kupanua fursa mbalimbali kwa vijana ikiwemo upatikanaji wa ajira katika maeneo mbalimbali hapa nchini,kwamba mawaziri hao wataainisha kwa kutoa takwimu sahihi juu ya mafanikio hayo.

“ninapenda kuwaalika vijana wa mkoa wa Morogoro na mikoa ya jirani,kote nchini kushiriki kwenye kongamano hilo ambalo litatanguliwa na maandamano yatakayoanzia ofisi za CCM Mkoa wa Morogoro vilizopo eneo la sabasaba hadi ukumbi wa tanzanite uliopo mjini Morogoro”alisema

Aidha,katika kongamano hilo vijana watakapata fursa za kujadiliana mambo mbalimbali yaliofanywa na serikali ya chama cha mapinduzi ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Sanjari na hilo,alisema kuwa kongamano hilo litashirikisha  Mawaziri wa sekta mbalimbali,viongozi mbalimbali wa serikali,asasi za kiraia ambao watapata fursa ya kuelezea mafanikio yaliopatikana katika kipindi cha miaka 4 ya uongozi wa serikali ya awamu ya sita hususan kwa upande wa vijana.

Alitaja Kauli mbiu ya Kongamano hilo ni “Wasomi Tumekuelewa Maendeleo Tumeyaona Dk Samia Mgombea wetu” kwamba katika kudhihirisha umuhimu wa kongamano hilo makundi mbalimbali yatashiriki wakiwemo mama na baba lishe,bodaboda,wafanyabiashara ndogondogo ‘wamachinga’ na asasi.

Kwa upande wake,Katibu wa umoja wa vijana CCM mkoa wa Morogoro,Vaileth Soka amewahimiza vijana wanawake kushiriki katika kongamano hilo ambalo linatoa taswira ya umoja na mshikamano katika jamii kwa kuwa mahitaji ya vijana yanafanana bila ya kujali itikadi ya mtu.

Katibu wa umoja wa vijana CCM mkoa wa Morogoro,Vaileth Soka(kushoto) akiwa katika mkutano na waandishi wa habari mjini Morogoro

Soka alisema ya kuwa katika kipindi cha serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuna mafanikio makubwa katika kada ya wanawake kwani zipo fursa nyingi zimeelekezwa kwa wanawake,hivyo muda wa kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi mkuu wajitokeze na kuchagua viongozi wanaowataka katika kuimarisha demokrasia hapa nchini.

No comments:

Post a Comment