Na Mwandishi wetu
Mamlaka ya hali ya hewa imeendelea kutoa tahadhari ikiwataka wananchi kuchukua hatua za mapema kukabiliana na El-Nino ambayo wamekuwa wakiifuatilia kwa ukaribu zaidi ikitajwa kuwa kubwa kati ya zilizowahi kutokea.
Kwa muujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), DR. Ladislaus Chang’a, Amesema katika historia baadhi ya El-Nino ambazo zilikuwa na nguvu kubwa ni ya 1982 -1983, 1997-1998, 2015-2016, na 2023-2024 na hii ambayo wanaendelea kuifuatilia 2026 tayari imefikia kiwango cha El Nino yenye nguvu kubwa kuelekea Oktoba itakuwa na nguvu kubwa zaidi.
Ametaja baadhi ya maeneo ambayo yataathirika kupata mvua za juu ya wastani ni pamoja na mikoa ya ukanda wa ziwa Viktoria (Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Simiyu, Mara), mvua zikitarajiwa kuanza wiki ya nne ya mwezi septemba.
Ukanda wa nyada za Juu Kaskazini Mashariki (Kilimanjaro, Arusha na Manyara) ametaja kupata mvua za juu ya wastani hadi wastani mvua zikitarajiwa kuanza wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba.
Ukanda wa Pwani ya Kaskazini (Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Kaskazini mwa mkoa wa Morogoro, visiwa vya Mafia) yatarajiwa kupata mvua za juu ya Wastani hadi wastani).

No comments:
Post a Comment