Breaking News

Sep 1, 2026

TANZANIA NA UJERUMANI ZAIMARISHA USHIRIKIANO UHIFADHI WA BIOANUWAO



Tanzania na Ujerumani Zaimarisha Ushirikiano wa Uhifadhi wa Bioanuwai

Na Mwandishi wetu

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi akiwa na Mwenyekiti Mwenza ambaye ni Mkuu wa Ushirikiano katika Ubalozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bi. Julia Kronberg wameongoza Kikao cha 13 cha Kamati ya Uendeshaji Steering Commitee) wa Miradi inayotekelezwa kwa ushirikiano baina ya Serikali ya Ujerumani na Tanzania.

Kikao hicho kimepokea na kujadili  taarifa za utekelezaji wa miradi mbalimbali inayofadhiliwa na serikali ya Ujerumani kupitia Benki ya maendeleo ya Ujerumani (KFW). Miradi hiyo inatekelezwa katika maeneo ya ikolojia za Serengeti, Katavi, Mahale na Selous Nyerere. 


Vilevile kikao hicho kimejadili  masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Ujerumani katika uhifadhi wa bioanuwai, usimamizi endelevu wa rasilimali za asili na kulinda mifumo ya ikolojia nchini.

Ushirikiano huo ni sehemu ya juhudi za pamoja za kuhakikisha utajiri wa bioanuwai wa Tanzania unaendelea kulindwa na kutumika kwa manufaa ya vizazi vya sasa na vijavyo.

Kikao hicho kimefanyika leo Septemba 1, 2026 katika Chuo cha Utalii jijini Dar es salaam.

No comments:

Post a Comment