Na Thadei Hafigwa
WANANCHI waliofika kutembelea banda la Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) katika Tamasha la Nne la Taifa la Utamaduni mkoani Morogoro wameonyesha shauku kubwa ya kupata elimu kuhusu shughuli za utafutaji, uchimbaji na uendelezaji wa rasilimali za mafuta na gesi asilia nchini.
Shauku hiyo ilijitokeza baada ya
wananchi mbalimbali kufika katika banda
Baadhi ya wananchi hao,ni Charles Pangapanga,Mkulima wa skimu ya Umwagiliaji Mvomero abaye alihoji iwapo tayari kuna uhakika wa uwepo wa mafuta nchini na ni lini shughuli rasmi za uchimbaji zinaweza kuanza.
Mjiolojia kutoka PURA, Lukelo Matimbwi, alisema kuwa bado kuna tafiti na shughuli za utafutaji zinazoendelea katika maeneo mbalimbali nchini ili kubaini uwepo na kiwango cha rasilimali za mafuta.
Alisema kuwa hadi sasa,
Matimbwi alieleza kuwa elimu inayotolewa na PURA inalenga kuwawezesha wananchi kuelewa nafasi ya mamlaka hiyo katika kusimamia na kudhibiti shughuli za mkondo wa juu wa petroli, zikiwemo shughuli za utafutaji na uendelezaji wa mafuta na gesi asilia.
Aidha, wananchi waliofika katika
banda
Tamasha la Nne la Taifa la Utamaduni, linaloendelea katika Viwanja vya Jamhuri mkoani Morogoro, limeendelea kuwa jukwaa muhimu kwa taasisi mbalimbali za serikali na wadau wengine kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu, huduma na fursa zinazopatikana katika sekta mbalimbali.
Kwa upande wake,Chifu wa Morogoro,Musa Lukwele amezipongeza Taasisi za serikali ambazo zimeshiriki katika Tamasha la Utamaduni limefanya uamuzi wa kizalendo,na kutoa elimu huduma wanazotoa kwa wananchi,na tafiti mbalimbali zinazofanywa na wataalamu katika kuharakisha maendeleo ya nchi.
Chifu Lukwele,alisema kuwa Machifu na Wazee wa Mila,pamoja na majukumu yao mengine wataendelea kutoa ushirikiano kwa serikali na watafiti watakapofika maeneo yao ya kiutawala ili kusipatwe vikwazo katika majukumu yao ya kuwaletea maendeleo yao.




No comments:
Post a Comment