KATIBU Mkuu
wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Gerson Msigwa, amesema
Tanzania inakabiliwa na changamoto ya mmomonyoko wa maadili, hali ambayo
imeifanya serikali kutoa nafasi kubwa kwa viongozi wa kimila, wakiwemo Machifu,
kushiriki katika juhudi za kusimamia na kuenzi maadili na utamaduni wa
Mtanzania.
Msigwa, ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, alisema
hayo Agosti 29, 2026, wakati akifunga Tamasha la Nne la Kitaifa la Utamaduni
lililofanyika katika Viwanja vya Jamhuri mkoani Morogoro.
Tamasha
Alisema kasi ya utandawazi na maendeleo ya teknolojia
imeleta changamoto katika uhifadhi wa utamaduni wa Tanzania, hivyo kuwepo kwa
umuhimu wa jamii, viongozi wa kimila na vyombo vya habari kushirikiana
kuhakikisha mila, desturi na maadili mema yanaendelea kuhifadhiwa na kurithishwa
kwa vizazi vijavyo.
“Leo hii nchini kwetu kijana mdogo kumtukana mtu mzima
inaonekana ni kitu cha kawaida. Mimi ni baba na mtoto wangu wa kwanza ana umri
wa miaka 25, lakini cha kusikitisha ni kwamba anashuhudia watoto wadogo
wakinitukana mitandaoni,” alisema Msigwa.
Katika kuelezea changamoto za matumizi mabaya ya
mitandao ya kijamii, Msigwa alisema hata yeye amewahi kukumbana na taarifa za
uongo zilizosambazwa mitandaoni kuhusu familia yake.
Alisema wakati akiwa njiani kuelekea kwenye tamasha
“Hata nilipokuwa nakuja hapa nilikuwa napokea pole
nyingi kwa sababu kuna watu wameandika mitandaoni kuwa mama yangu amefariki.
Nataka niwaambie kuwa mama yangu hajafa, ni mzima wa afya na yupo kijijini
Iringa anaendelea na shughuli zake
Msigwa alisema moja ya dhamira ya serikali ni
kuhakikisha utamaduni wa Mtanzania unarithiwa na vizazi vya sasa na vijavyo kwa
kuwa unafundisha misingi ya kuheshimiana, kusaidiana na kupendana.
Aidha, aliwataka wadau wa utamaduni kujenga mazingira
yatakayowezesha bunifu mbalimbali kustawi na kutumika
Kupitia tamasha



No comments:
Post a Comment