SUGECO YABAINISHA VIJANA 850 WANUFAIKA NA USHIRIKIANO NA NCHI ZA NORDIC
Na Thadei Hafigwa,Morogoro
TAASISI ya Wajasiriamali Wahitimu wa Chuo Kikuu cha
Kilimo cha Sokoine (SUGECO) kimefungua ukurasa mpya wa maendeleo kwa vijana na
wanawake nchini kupitia mpango kabambe wa ushirikiano kati yake na nchi za
Nordic ambazo ni Denmark, Finland, Norway, na Sweden.
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo(SUA),Prof.Raphael Kibunda ameonesha shukran zake kwa nchi za Nordic kwa kusaidia Chuo Kikuu cha Sokoine Cha Kilimo katika ukuzaji na uendelevu wa kitaaluma katika programu mbalimbali za kubadilishana uzoefu.
Prof.Kibunda ametaja nchi ya Denmark imekuwa ni nchi ya kwanza kufadhili ndaki ya tiba ya mifugo,ambapo kwa walikuwa wakileta walimu kwenye tiba ya wanyama kwa kuwafundisha wanafunzi chuoni hapo,ambapo kwa sasa wanaendelea vizuri.
"tunawashukuru kwa kipindi chote hicho,kwa sasa tumesimama wenyewe,tuna walimu wetu wenyewe,tumekubaliana tuwe na uwezo wa kubadilishana wanafunzi na pia kubadilishana walimu."alisema Prof.Kibunda.
kwa upande wake,Balozi wa Denmark Nchi Tanzania,Jesper Kammersgaard,alisema kuwa Nchi za Nordic zimekuwa na utarabu wa kukuza ujasiriamali katika kilimo,ambapo wameweza kukutana na vijana 20 katika Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo(SUA) ambao waliwahi kujifunza ujuzi nchini Denmark ambao wamerudi Tanzania ili kujua namna wanavyotumia ujuzi na maarifa waliyapata wakiwa nje ya nchi.
Kwa
mujibu wa taarifa ya Mkurugenzi Mtendaji wa SUGECO, Revocatus Kimario kwa
Ubalozi wa Nchi za Nordic waliotembelea Taasisi hiyo iliopo ndani ya Chuo Kikuu
cha Sokoine (SUA) ambayo inafadhiliwa na
nchi hizo za Nordic ambapo katika kipindi cha miaka miwili,jumla ya
vijana 850 kutoka chuo kikuu wamenufaika na Programu ya kujifunza nje ya nchi katika nchi hizo.
Kimario
alibainisha kuwa SUGECO inalenga kushirikiana na taasisi na vyuo vikuu kutoka
nchi hizo katika maeneo mbalimbali muhimu ya maendeleo endelevu, ikiwa ni
pamoja na elimu, ujasiriamali, uhifadhi wa mazingira, na teknolojia ya kisasa
ya kilimo na mifugo.
Mikakati
ya Kuwezesha Vijana na Wanawake
SUGECO
inatilia mkazo ushirikiano katika nyanja ya elimu kwa kupendekeza mpango wa
kubadilishana wanafunzi na programu za mafunzo kwa vitendo (internship), pamoja
na kuanzisha shahada ya pamoja ya "sandwich" kati ya Chuo Kikuu cha
Kilimo cha Sokoine (SUA) na vyuo vya Nordic. Lengo ni kuongeza ujuzi na uzoefu
wa kimataifa miongoni mwa vijana wa Kitanzania katika sekta ya kilimo, misitu,
na biashara endelevu.
Aidha,
taasisi hiyo inapendekeza kuanzishwa kwa mfuko wa maendeleo kwa wajasiriamali
vijana na wanawake kwa kushirikiana na taasisi za maendeleo kutoka Nordic.
Mfuko huo utasaidia vijana waliomaliza mafunzo kwa vitendo kuingia katika
biashara zenye tija, huku pia ukianzisha mfumo wa kifedha wa mzunguko kwa ajili
ya biashara zinazoongozwa na vijana.
Katika
hatua nyingine, Youth Acceleration Program ya SUGECO inalenga kusaidia
biashara changa zinazoongozwa na vijana kwa kuzikuza, kuzilea na kuzihusisha na
masoko, kwa kushirikiana na makampuni ya Nordic katika kutoa msaada wa kifedha,
kiufundi na kiushauri.
Uhifadhi
wa Mazingira na Teknolojia ya Kisasa ya Mifugo
Katika
kuunga mkono jitihada za kimataifa za uhifadhi wa mazingira, SUGECO inakusudia
kushirikiana na Bamboo Village Trust kutoka Indonesia pamoja na
wataalamu wa Nordic kuendeleza mradi wa uhifadhi wa mianzi nchini. Mradi huu
pia utahusisha kubadilishana wanafunzi kati ya SUA na vyuo vya Nordic katika
masuala ya misitu na usimamizi wa rasilimali endelevu.
Kwa
upande wa teknolojia ya kisasa ya mifugo, SUGECO imeingia ubia na kampuni ya
Danben kutoka Denmark kuanzisha kituo cha kisasa cha uhimilishaji bandia wa
nguruwe. Mradi huu utasaidia kuongeza tija kwa wakulima wadogo, kuboresha
vinasaba vya mifugo, na kutoa ajira na mafunzo kwa vijana katika teknolojia za
kisasa za ufugaji.
Manufaa
kwa Nchi Washirika
Kwa
mujibu wa SUGECO, nchi za Nordic zitafaidika kwa kuimarisha uhusiano wa kielimu
na kiteknolojia na Tanzania, kupata fursa za uwekezaji katika masoko
yanayoibukia, na kushiriki moja kwa moja katika kufanikisha malengo ya
maendeleo endelevu duniani.
“Tunayo
matumaini makubwa kwamba ushirikiano huu utaleta mabadiliko chanya ya muda
mrefu kwa vijana, wanawake, jamii, na mazingira kwa ujumla,” imeeleza sehemu ya
taarifa hiyo. “Tunasubiri kwa hamu kujadiliana kwa kina juu ya fursa hizi na
kupata msaada wa wenza wetu ili kufanikisha malengo haya ya pamoja.”
Kwa
mafanikio haya, SUGECO inaendelea kudhihirisha kuwa taasisi muhimu katika
kuibua na kukuza vipaji vya vijana wa Kitanzania na kuwaunganisha na fursa za
kimataifa kwa maendeleo jumuishi na endelevu.


No comments:
Post a Comment