Ziara ya Waziri wa Ujenzi yaonyesha dhamira ya Serikali kumaliza kero za barabara na madaraja Morogoro
Na Thadei Hafigwa
Kwa miaka mingi, wakazi wa Mlimba, Malinyi na Ulanga
mkoani Morogoro wameendelea kuishi na changamoto ya miundombinu duni ya
barabara, hali inayokwamisha shughuli za kiuchumi, huduma za afya, elimu na
usafirishaji wa mazao. Kipindi cha mvua kimekuwa kikiambatana na adha ya
kukatika kwa mawasiliano kutokana na ubovu wa barabara na ukosefu wa madaraja
ya kudumu.
Hata hivyo, ziara ya Waziri wa Ujenzi, Abdallah Hamis Ulega, katika maeneo hayo imeibua matumaini mapya kwa wananchi baada ya Serikali kuonyesha msimamo mkali dhidi ya ucheleweshaji wa miradi ya ujenzi na kusisitiza utekelezaji wa haraka wa miradi ya kimkakati.
Miongoni mwa miradi iliyozua mjadala mkubwa ni ujenzi wa
barabara ya Ifakara–Mbingu yenye urefu wa kilometa 62.5,
ambayo ni kiungo muhimu cha uchumi katika Jimbo la Mlimba.
Licha ya Serikali kusaini mkataba na kampuni ya
Barabara hiyo ni muhimu kwa kuwa inapita katika maeneo
yenye uzalishaji mkubwa wa mpunga, mahindi, ufuta, mbao na mazao mengine ya
biashara yanayochangia uchumi wa Mkoa wa Morogoro na Taifa kwa ujumla.
Mbunge wa Mlimba apaza sauti
Katika ziara hiyo, Mbunge wa Jimbo la Mlimba, Dkt.
Kellen Rosemary Rwakatare, aliwasilisha kwa Waziri changamoto
zinazowakabili wananchi kutokana na kuchelewa kwa mradi huo.
Alieleza kuwa wananchi wameendelea kupata hasara kubwa
kutokana na ubovu wa barabara, huku gharama za usafiri zikiongezeka na
usafirishaji wa mazao kwenda masokoni kuwa mgumu.
Mbunge huyo aliiomba Serikali kuchukua hatua za haraka
ili kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na kuondoa adha ambayo
wananchi wameivumilia kwa muda mrefu.
Serikali yatoa onyo kali kwa mkandarasi
Akizungumza wakati wa ukaguzi wa mradi huo, Waziri wa
Ujenzi, Abdallah Ulega, alionyesha kutoridhishwa na kasi ya utekelezaji wa kazi
licha ya Serikali kutimiza wajibu wake wa kifedha.
Alisema Serikali haiwezi kuvumilia hali ya kucheleweshwa
kwa miradi ya maendeleo inayogusa maisha ya wananchi.
"Hivi hamuoni namna wananchi wanavyoumia? Serikali
imeshatoa fedha lakini maendeleo ya mradi hayaendani na makubaliano ya mkataba.
Hili hatuwezi kulivumilia."
Waziri Ulega alisema utekelezaji wa mradi huo umefikia
takribani asilimia tano pekee, kiwango ambacho hakilingani na fedha
zilizokwisha kulipwa.
Kutokana na hali hiyo, alitoa muda wa wiki moja kwa
wataalamu wa Wizara ya Ujenzi na TANROADS kufanya kikao na viongozi wa kampuni
ya Henan Railway ili kujadili hatma ya mradi huo.
Alisisitiza kuwa iwapo mkandarasi hataonyesha uwezo wa
kutekeleza wajibu wake kwa mujibu wa mkataba, Serikali haitasita kuuchukua
hatua ikiwemo kuvunja mkataba na kuifungia kampuni hiyo kushiriki miradi
mingine nchini.
Serikali ya Samia yaongeza kasi ya uwekezaji
Ziara ya Waziri Ulega imekuja wakati Serikali ya Awamu
ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiendelea kuongeza uwekezaji
mkubwa katika sekta ya miundombinu.
Katika Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Ujenzi ya
mwaka wa fedha 2026/2027, Serikali imeweka kipaumbele katika kujenga
na kukarabati barabara za kitaifa, kujenga madaraja ya kudumu pamoja na kuhakikisha
barabara zinapitika katika kipindi chote cha mwaka.
Mkakati huo unalenga kuunganisha maeneo ya uzalishaji na
masoko, kupunguza gharama za usafiri, kuongeza biashara na kuvutia wawekezaji.
Changamoto za Ulanga na Malinyi
Mbali na Mlimba, Waziri Ulega alitembelea pia wilaya za
Ulanga na Malinyi kukagua maeneo yatakayojengwa madaraja.
Katika ziara hiyo, Mbunge wa Jimbo la Ulanga, Salim
Alaudin Hasham, aliwasilisha changamoto za wananchi zinazotokana na ubovu wa
barabara na madaraja, hususan katika kipindi cha mvua ambapo baadhi ya vijiji
hukatika mawasiliano kwa siku kadhaa.
Alieleza kuwa wananchi wanaendelea kuiunga mkono
Serikali lakini wanatarajia kuona utekelezaji wa miradi ukienda kwa kasi zaidi
ili kuondoa changamoto hizo.
Adam Malima: Morogoro ni mkoa wa kimkakati
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Adam Malima, alisema Morogoro
ni miongoni mwa mikoa muhimu zaidi kiuchumi nchini kutokana na kuunganisha
maeneo mengi ya uzalishaji wa kilimo na mtandao wa barabara za kitaifa.
Alisema Serikali imeendelea kushirikiana na Wizara ya
Ujenzi, TANROADS na TARURA kuhakikisha changamoto za miundombinu zinapatiwa
ufumbuzi wa kudumu.
Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Mkoa, ujenzi wa madaraja
katika maeneo yenye
Miundombinu ni injini ya uchumi
Wataalamu wa uchumi wanaeleza kuwa uwekezaji katika
barabara na madaraja huongeza uzalishaji wa kilimo, hupunguza gharama za
usafirishaji, huvutia uwekezaji na kuongeza ajira.
Kwa Mkoa wa Morogoro, ambao ni miongoni mwa wazalishaji
wakubwa wa mazao ya kilimo nchini, barabara bora zina maana ya kuongeza
ushindani wa mazao katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Matumaini mapya
Ziara ya Waziri Abdallah Ulega imeonyesha kuwa Serikali
haitaki kuona miradi ya maendeleo ikikwama kutokana na uzembe wa wakandarasi.
Hatua ya kutoa onyo kali kwa mkandarasi wa barabara ya
Ifakara–Mbingu pamoja na kuendelea kusimamia ujenzi wa madaraja katika Ulanga
na Malinyi imeongeza matumaini kwa wananchi kuwa kero za muda mrefu za
miundombinu zinaelekea kupata ufumbuzi.
Iwapo maelekezo yaliyotolewa yatatekelezwa kwa wakati, siyo tu kwamba
Mlimba, Malinyi na Ulanga zitafunguka kiuchumi, bali Mkoa wa Morogoro
utaendelea kuimarisha nafasi yake

No comments:
Post a Comment