Breaking News

Jan 30, 2021

RC PWANI ALITAKA JESHI LA POLISI KUDHIBITI UHARIFU


MKUU WA MKOA WA PWANI,MHANDISI EVARISTI NDIKILO


RC PWANI ALITAKA JESHI LA POLISI KUDHIBITI UHARIFU

NA VICTOR MASANGU, PWANI

MKUU wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evarist Ndikilo, amelitaka jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kuhakikisha kwamba  linaweka mikakati madhubuti kwa ajili ya kuthibiti wimbi la uharifu pamoja na kukomoshe matumizi ya madawa ya kulevya ikiwemo bangi pamoja na unywaji wa pombe haramu ya gongo ambayo ina madhara makubwa kwa afya ya binadamu.

Ndikilo, ametoa kauli hiyo, wakati akizungumza na  askari wa jeshi la polisi kutoka wilaya mbalimbali za Mkoa wa Pwani, wakati wa sherehe maalumu iliyoandaliwa kwa ajili ya kuuaga mwaka wa 2020 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2021, pamoja na  kuweza kupanga mikakati ya kulinda hali ya ulinzi na amani pamoja na kujadili changamoto zilizopo kwa askari polisi ili kuweza kuzitafutia ufumbuzi.

Ndikilo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama mkoa, alisema kuwa kumekuwepo kwa baadhi ya maeneo bado kuna baadhi ya watu wanajichukulia sheria mikononi na kusababisha uvinjifu wa amani hivyo alimuagiza Kamanda wa polisi Mkoa wa Pwani kuhakikisha kwamba analilisimamia suala hili kikamilifu na kuongeza zaidi doria katika maeneo mbali mbali lengo ikiwa ni kuimarisha hali ya ulinzia kwa wananchi.

“Mimi kama Mkuu wa Mkoa wa Pwani nashukuru sana kupata mwaliko katika sehehe hizi ambazo zimeandaliwa na jeshi la polisi lakini kitu kikubwa ninachowaomba ni lazima sasa kuweka mipango mizuri ya kutekeleza wajibu wetu ipasavyo maana katika baadhi ya maeneo bado kuna watu wanaendelea kufanya vitendo vya uharifu hivyo ni lazima kuwabaini wale wote ambao wanahatarisha uvunjifu wa amani na wakamatwe na wachukuliwe hatua kali za kisheria,”alisema Ndikilo.

Aidha, Ndikilo, alibainisha kwamba, anachukizwa sana kuona bado kuna baadhi ya wananchi wanandelea kutumia pombe aina ya kongo ambayo ni haramu, hivyo ameliagiza jeshi hilo kufanya msako mkali kwa ajili ya kuwakamata wale wote ambao watakutwa wanatumia pombe hiyo wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria na taratibu za nchi.

Kadhalika, alisema kuwa serikali ya awamu ya tano, lengo lake kubwa ni kuhakikisha kwamba inaweka misingi imara katika kulinda nchi yake katika sehemu mbalimbali, hivyo, askari wa jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola waendelee kufanya doria za mara kwa mara katika mipaka ili kuthibiti waharifu na watu wengine wasiingie nchini kinyemela na kuja kufanya uharifu.

“Kumekuwepo na wimbi la wahamiaji haramu ambao wanaingia nchini kinyemela pasipo kuzingatia sheria na taratibu, naliagiza jeshi la polisi pamoja na maafisa mbalimbali wa ulinzi kuhakikisha  wanalinda mipaka ya nchi ya sehemu nyingine ambazo baadhi ya raia wa kigeni wanatumia njia hizo katika kupita na kuingia nchini hasa katika maeneo ya bandari bubu kama vile maneo ya Wilayani Bagamoyo,”aliongeza Ndikilo.

Pia, katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa alilipongeza jeshi la polisi Mkoa wa Pwani kwa kuweza kuweka mikakati ya kupunguza ajali za barabarani kwa kiwango kikubwa na kuwataka watumiaji wa vyombo  vya usafiri kuhakikisha kwamba wanazingatia sheria zote za barabarani ili kuepukana na ajali ambazo zinapelekea watu kupoteza maisha yao na wengine kupata ulemavu.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Wankyo Nyigesa alimahidi Mkuu huyo wa mkoa wa Pwani, kuzishughulikia changamoto mbalimbali zilizopo na kwamba ataendelea zaidi kulivalia njuga suala la wimbi la uharifu kwa lengo la kudumisha hali ya ulinzia na usalama.

 

No comments:

Post a Comment