Breaking News

Jul 16, 2026

Morogoro Yaongeza Kasi ya kuvutia Wawekezaji yaweka mpango Mahususi

 KATIBU TAWALA MKOA WA MOROGORO,DKT.MUSSA ALI MUSSA AKISISITIZA JAMBO

Morogoro Yaongeza Kasi ya kuvutia Wawekezaji yaweka mpango Mahususi

Na Mwandishi wetu

KATIKA kuhakikisha ya kuwa fursa za uwekezaji zinaeleweka kwa wanda mpana Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Mussa Ali Mussa amewataka wataalamu na Taasisi zilizopo Mkoa wa Morogoro kuzielewa na kuzitambua fursa hizo ili ziweze kutangazwa na kufahamika kwa wawekezaji, wanachi na wadau wa maendeleo.

‎Akifungua kikao cha uhuishaji wa Muongozo wa fursa za uwezekezaji,Dkt Mussa amebainisha kwamba  ili mpango huo uweze kutambulika na kueleweka wataalamu wa Mkoa huo wanapaswa kufahamu fursa za uwekezaji zilizopo katika njanya mbali mbali ikiwmo kilimo,utalii biashara na ufugaji pamoja na fursa za usafirishaji zilizopo ikwemo reli ya mwendo kasi (SGR).


‎"Morogoro tuna fursa nyingi tumezieleza?  " amesema Dkt. Mussa.

‎ Dkt Mussa ametoa wito huo,Julai 15,mwaka huu, ametaka utekelezaji wa mpango huo kushirikisha  wanachi sio tu kufahamu fursa zilizopo pia kuwa sehemu ya utekelezaji wa mpango huo ili uwe na manufaa kwa jamii husika.

Aidha,Alisema kuwa mkoa wa Morogoro umejaliwa kuwa na rasilimali na fursa nyingi ambazo bado hazijatangazwa kwa kiwango kinachostahili.

‎Kwa upande wake, Mkuu wa sehemu ya Viwanda,Biashara na Uwekezaji,  Mkoa wa Morogoro Bi. Beatrice Njawa amesema kuwa muongozo uliopo   umepitwa na wakati hivyo unahitajika  kuhuishwa  na kujengewa uwelewa kwa Taasisi na Sekretariet ya Mkoa ili uweze kueleweka  na hatimaye kutangaza  fursa za uwekezaji  zilizopo  kwa jamii.

‎Naye, Dkt Hoseana Lunogelo ambaye ni Mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa  Kiuchumi na kijamii Tanzania ( ESRF),  amesema kuwa wao kama Taasisi wanashughulikia masuala ya utafiti kwa upande wa Serikali na Sekta binafsi hivyo  Mikoa yote inahitajika  kuandaa na  kuanisha fursa  za vivutio vya  uwekezaji vilipo kwenye maeneo yao  ukiwemo Mkoa wa Morogoro.

‎Dkt Lunogelo  amesema kuwa kama Taasisi wanasaidia Kufanya utafiti katika nyanja  za  uchumi jumuishi, utandawazi, utawala bora, rasilimali asilia pamoja na kuimarisha uchumi wa kidijitali ambapo masuala ya fursa za vivutio vya uwekezaji vinafanyiwa kazi.

No comments:

Post a Comment