Breaking News

Mar 14, 2025

DOYO WA NLD ALETA FUKUTO LA KINYANG’ANYIRO CHA URAIS NDANI YA CHAMA CHAKE

 

Doyo Hassan Doyo(Pichani) Akisisitiza jambo wakati alipoongea na waandishi wa habari mjini Morogoro kuhusu dhamira yake ya kugombea urais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama chake cha NLD.

DOYO WA NLD ALETA FUKUTO LA KINYANG’ANYIRO CHA URAIS NDANI YA CHAMA CHAKE

Na Thadei Hafigwa

WAKATI vyama vingine vya siasa vikijiweka mguu sawa kuelekea uchaguzi mkuu wa Urais,Ubunge na Udiwani hapa nchini unaotarajia kufanyika Oktoba mwaka huu mwanachama wa Chama cha Nation League for Democracy (NLD), Doyo Hassan Doyo amekutana na waandishi wa habari na tangaza nia ya kugombea nafasi ya urais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Doyo amebainisha  vipaumbe 10 ambavyo kwa mtazamo wake iwapo akipitishwa na chama chake ndivyo akavyovinadi kwa watanzania kwenye majukwaa ya siasa kuomba ridhaa ya kuchaguliwa kuwa rais wa Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini Morogoro Machi 14.2025, Doyo ametaja vipaumbele hivyo ni ajira, elimu, kilimo na ufugaji, rasilimali za maji, kuziba mianya ya ukwepaji wa kodi.

Kipaumbele vingine ni pamoja na  kupambana na rushwa kwa kiwango kikubwa na kujenga taifa la walipa kodi kwa kiwango kinachostahili,hata hivyo amechukua fursa hiyo kuipongeza mamlaka ya mapato nchini kwa jitihada zake za kukusanya mapato.

Aidha,Doyo kwa mtazamo wake haoni sababu ya chama chake kuungana na vyama vingine kuing’oa CCM madarakani kwa kuwa chama hicho kimesheni wanachama wenye sifa na uweledi wa kushika dola.

Amesema kuwa chama chake kitasimamisha wagombea ubunge nchini nzima na pia baadhi ya maeneo watasimamia wagombea katika nafasi ya udiwani kwa kuwa wamejipanga vema katika kuhakikisha wapiga kura wao wamejiandikisha katika daftari la kudumu la kupika kura.

“iwapo nikipitishwa na chama change kuwa mgombea,kipaumbe change kikubwa ni kupambana na suala ajira ambayo limekuwa ni tatizo kubwa tunao wasomi wamemaliza vyuo vikuu lakini hawajapata ajira rasmi baadhi yao wanajihusisha na sekta ya usafirishajiwa abiria kwa bodaboda”alisema na kuongeza kuwa

“siibezi ajira ya bodaboda bali mazingira waliokuwa nayo wasomi wetu waliohitimu vyuo vikuu kwa kujihusisha na shughuli za bodaboda inapunguza hadhi ya elimu yetu hapa nchini.”

Mbali na hayo amejinasibu kwa kuweka vipaumbele vingine ni pamoja na kuweka nguvu katika sekta ya madini, kuongeza jitihada kwa watoto wa kike katika kupata elimu ya teknolojia.

Kadhalika kwa mtazamo wake amesema atahakikisha wanaimarisha Muungano wa Tanzania na kuimarisha sekta ya binafsi katika kukuza na kuongeza tija katika shughuli za kiuchumi  kwa wananchi kwa kutumia rasilimali zilizopo ikiwemo sekta ya madini.

Pia,hakusita kutaja baadhi ya mafanikio yaliyopatikana katika serikali ya awamu ya sita ikiwemo SGR,bwawa la kufua umeme la Mwalimu Julius Nyerere,ujenzi wa vyuo vikuu nchi ambapo wakati taifa lililopata uhuru kulikuwa na chuo kikuu kimoja.

Katika mkutano huo, Doyo aliongozana meneja wake, Twaha Saidi Mngatwa na familia yake, mkuu wa itifaki, Kibi Saidi Amri.Kwa upande wake Twaha Saidi Mngatwa meneja wa mtia nia (mgombea),

 amebainisha kuwa baada ya kutangaza nia ya bosi wake kugombea nafasi ya urais atachukua fomu katika chama chake Machi 21 na ifikapo April 10 kutafanyika uteuzi ndani ya chama atapeperusha bendera ya kunadi sera za chama katika mikutano ya kampeni baada ya kupitishwa na tume huru  taifa ya uchaguzi.

 

 

No comments:

Post a Comment